WAANDISHI wetu
KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackson Nyambele (28) mkazi wa Mbezi Mtoni jijini Dar, amefariki dunia baada ya kusombwa na maji ya mto uliopo Mbezi alipokuwa akifanya masihara na wenzake.Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Machi 22, mwaka huu ambapo chanzo chetu makini kinadai kuwa, awali marehemu alikuwa akibishana na wenzake kwamba yeye anaweza kuvuka kwenye mto huo mwingine akiweka dau kuwa, atakayeweza kuvuka atampa pesa.
KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackson Nyambele (28) mkazi wa Mbezi Mtoni jijini Dar, amefariki dunia baada ya kusombwa na maji ya mto uliopo Mbezi alipokuwa akifanya masihara na wenzake.Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Machi 22, mwaka huu ambapo chanzo chetu makini kinadai kuwa, awali marehemu alikuwa akibishana na wenzake kwamba yeye anaweza kuvuka kwenye mto huo mwingine akiweka dau kuwa, atakayeweza kuvuka atampa pesa.
“Walipokuwa wakibishana kuhusu kuvuka mto ule na mwenzao mmoja kuahidi kuwa atakayevuka atapewa fedha, ghafla sehemu ya udongo aliokuwa amekanyaga Jackson ulimomonyoka na kumfanya ateleze na kutumbukia mtoni.
“Hakuna aliyeweza kumsaidia kwa sababu maji yalikuwa mengi na ya kasi sana huku yakiwa na matakataka kiasi kwamba hata kama unaweza kuogelea, ni vigumu kuyamudu,’’ kilidai chanzo hicho.
Ikaelezwa kuwa, baada ya kufuatiliwa ndipo mwili wake ukakutwa ufukweni mwa bahari huko Kunduchi ukiwa umejaa maji.
Ikaelezwa kuwa, baada ya kufuatiliwa ndipo mwili wake ukakutwa ufukweni mwa bahari huko Kunduchi ukiwa umejaa maji.
Akizungumza na waandishi wetu, Mwenyekiti wa Mtaa anaoishi Jackson, Rehema Muya alisema tukio hilo ni la kusikitisha na mto huo miaka ya hivi karibuni umeua watu wapatao 10 katika mazingira ya kutatanisha.
Mwili wa marehemu Jackson umezikwa Jumanne iliyopita katika makaburi ya Mbezi Juu. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amen.
Mwili wa marehemu Jackson umezikwa Jumanne iliyopita katika makaburi ya Mbezi Juu. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amen.
0 comments:
Post a Comment